Makambako, Njombe – 28 Novemba 2025
Katika Ibada maalum iliyofanyika Usharika wa Makambako KKKT Dayosisi ya Kusini imemsimika rasmi Mchungaji BOAZ JAPHET MBILINYI kuwa Mkuu wa jimbo la Makambako. Tukio hili la kihistoria lilihudhuriwa na viongozi wakuu wa makanisa, wachungaji wa sharika mbalimbali, pamoja na waumini kutoka sehemu mbalimbali za jimbo hilo.
Ibada hiyo iliongozwa na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kusini Mhashamu Dk George Mark Fihavango akisaidiana na Msaidizi wa Askofu Mhashamu Dk Johnson Lunanilo Gudaga. Viongozi wengine waliojiunga na ibada hiyo ni Mkuu wa Seminari ya Kilutheri ya Kidugala, Mchungaji Wallace Lupenza pamoja na wachungaji washarika za jimbo la Makambako.






