Category Archives: Habari za jumla
Hazina ya KKKT Ilembula
Ndugu washiriki wote wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania:
Je, unajua KKKT ina hazina ya pekee sana – ukilinganisha na Makanisa mengine ya Kilutheri?
Si Ilembula tu, bali katika parokia zote.
Rafiki yetu Lufunyo kutoka Ujerumani aligundua hazina hizi kule Ilembula wakati wa ziara zake – labda utazijua baadhi yake! – na akatoa video.
Unaweza kuona hapa: Hazina katika Ilembula
Moto umeteketeza Jengo la Njombe lililopo Ilembula
Tarehe 7 Mei 2020:
Ajali ya moto mapema jioni – jengo limeharibiwa kabisa
Jengo hilo lilitumika kama mabweni ya wanafunzi wa ILVTC. Vitu vyote viliteketezwa. muda huu wanafunzi watakuwa wakiishi kwenye nyumba ya Mwinjilisti Kiginga ingawa inahitaji ukarabati na umeme.
Mnamo tarehe 14 Mei Mkutano wa ILVTC-Bodi na MAIL-kamati ulijadili kuhusu matokeo ya moto na shughuli zinazofuata. Picha unaweza kuona ⇒ hapa .
Februari 2021: Habari kuhusu ILVTC Fitting School Ilembula
Kwenye ukurasa ILVTC Fitting School Ilembula utapata picha na taarifa nyingi kuhusu Fitting School tangu ilipoanzishwa 2004 hadi leo!